Kama ilivyo ada wapendwa katika bwana leo nmewaandalia blog ambayo itakuwa ikizungumzia mambo kadha wa kadha kuhusu dini, utapata nyimbo mbalimbali za dini za kikristu na kiislamu.
utapata dondoo kedekede za maswali na majibu kutoka dini mbalimbali.
nmelenga zaidi kuwa weka sawa watu wengi wajifunze na kuelewa umhimu wa kuvumiliana katika dini (religious torelance). hii yote ni kutokana baadhi ya wengi wetu kujisahau kuwa sote tume umbwa na baba mmoja yaani ( Mungu) na hivyo ni wamoja. Awali ya yote ebu tuanze kutazama maana halisi ya neno dini.
DINI,
Dini (kutoka Kiarabu اﻟدﻴن, tamka: ad-din) inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji.
Ibada ni nguzo mojawapo iliyo dhahiri miongoni mwa dini kadhaa katika kuunganisha dhamira za mwenye kushika dini na mhimili wa imani, lakini dini inahusu pia mafundisho kuhusu maadili, mema na mabaya, imani na jinsi ya kushiriki katika jumuiya za waumini.
Kwa maana nyingine "dini" inataja jina kielelezo juu ya aina mbalimbali za imani jinsi inavyopatikana duniani, yaani jumuiya za kidini.
tazama nembo mbalimbali zinazo tumiwa na dini mbalimbali
Dini kama jumuiya kubwa
Dini kwa maana hiyo yenye wafuasi wengi duniani ni:Pamoja na hizi kuna dini mbalimbali zinazojulikana tangu karne nyingi duniani hata kama idadi ya wafuasi si kubwa sana kwa mfano:
- Uyahudi
- Uzardoshti (Uzoroaster)
- Ujain
- Usingasinga
- Dini asilia za Kiafrika
- Dini asilia za Kichina
- Ushamani
- naamini hadi apo umepata mwanga kuhusu dini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni